Ratiba ya Juma Linaloanza Novemba 1
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 1
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
cf sura ya 12 ¶15-21, sanduku kwenye uku. 127
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Mambo ya Nyakati 16-20
Na. 1: 1 Mambo ya Nyakati 17:1-10
Na. 2: Je, Dini Nyingine Zinafuata Biblia? (rs uku. 192 ¶4)
Na. 3: Maonyo Katika Maandiko Kuhusu Mambo Ambayo Lazima Wakristo Wayakimbie
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 12: Matangazo na Tunavumilia Majaribu Mbalimbali. Hotuba inayotegemea kitabu Tengenezo, ukurasa 176, fungu la 2, hadi ukurasa 178, fungu la 2. Mhoji kifupi mhubiri mmoja kuhusu mambo ambayo yanamsaidia kudumisha bidii katika utumishi licha ya matatizo makubwa ya afya.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Zungumza na wasikilizaji kuhusu vikumbusho vya arusi vinavyotegemea makala mbili zenye kichwa “Thibitisha Imani Yako Kupitia Maisha Yako” na “Ongeza Shangwe na Heshima ya Siku Yako ya Arusi” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 2006. Kazia mambo yafuatayo: Epuka mambo yanayofanywa kwa ajili ya kujionyesha tu, na roho ya kushindana. Epuka mambo ya kilimwengu katika muziki, kucheza dansi, au mambo mengine. Zingatia kiasi cha Kikristo katika mavazi na kujipamba hata kwa bwana na bibi-arusi. Uwe mwangalifu kwa sababu watu wa ukoo na hata watu wengine wanaweza kukushinikiza kufanya mambo kulingana na mapendezi yao na hasa ikiwa wanasaidia katika kugharimia karamu ya arusi. Acheni pindi yenye shangwe ya arusi imletee Yehova utukufu.—Mt. 5:16.
Dak. 8: Jitayarishe Kutoa Magazeti Mwezi wa Novemba. Mazungumzo. Tumia dakika moja au mbili kupitia magazeti ya karibuni. Onyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.