Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Kuanzia Novemba 2010 hadi Januari 2011, mapainia wa pekee wa muda 40 na wahubiri na mapainia wa kawaida 2,580 walishiriki katika kazi ya kuhubiri kwenye eneo la mbali. Waliwagawia watu jumla ya vitabu 6,738, vijitabu 17,203, magazeti 41,945, na wakaanzisha mafunzo ya Biblia 3,621. Ushahidi mkubwa sana ulitolewa katika kipindi hicho.