Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 29, 2011.
1. Fadhili zenye upendo za Yehova “ni bora kuliko uzima” katika njia gani? (Zab. 63:3) [w01 10/15 uku. 15 fu. 17]
2. Zaburi ya 70 inaonyesha nini kumhusu Daudi? [w08 9/15 uku. 4 fu. 4]
3. Zaburi ya 75:5 inatuonya kuhusu nini? [w06 7/15 uku. 11 fu. 3]
4. Ni wakati gani hasa tunapoweza kumtazamia Yehova asikilize sala zetu? (Zab. 79:9) [w06 7/15 uku. 12 fu. 5]
5. ‘Mambo yaliyofichika’ yanayotajwa katika Zaburi 90:7, 8 ni gani? [w01 11/15 uku. 12-13 fu. 14-16]
6. Kama inavyoonyeshwa katika Zaburi 92:12-15, Wakristo walio wazee kwa umri wamepewa jukumu gani katika kutaniko? [w04 5/15 uku. 13-14 fu. 15-18]
7. Je, maneno ya Zaburi 102:25-27 yanapinga kusudi la Mungu la milele kwa dunia? (Mwa. 1:28) [w08 4/1 uku. 12 fu. 1]
8. Tunajifunza nini kuhusu ufahamu katika Zaburi 106:7? [w95 9/1 uku. 19 fu. 4–uku. 20 fu. 2]
9. Kulingana na Zaburi 110:1, 4, Yehova anaapa nini kuhusu Uzao ulioahidiwa, au Masihi, na hilo litawaleteaje baraka wanadamu wote? [cl uku. 194 fu. 13]
10. Kutafakari faida za utumishi wake kwa Mungu kulikuwa na matokeo gani kwa mtunga-zaburi? (Zab. 116:12, 14) [w09 7/15 uku. 29 fu. 4-5]