Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Tulishuhudia ongezeko la utendaji katika mwezi wa Aprili. Wengi waliunga mkono utendaji wa painia msaidizi kama tulivyokuwa tumetiwa moyo. Kulikuwa na vilele vipya vya mapainia wasaidizi 6,920, saa 661,233, magazeti 285,011, ziara za kurudia 188,847 na mafunzo ya Biblia 41,410. Idadi ya wahubiri waliotoa ripoti mwezi wa Aprili ilikuwa 24,198. Hilo lilikuwa ongezeko la asilimia 6 na ndiyo idadi ya juu zaidi katika mwaka huo wa utumishi. Asilimia 42 ya jumla ya wahubiri walitumika wakiwa mapainia wasaidizi, mapainia wa kawaida, mapainia wa pekee au wamishonari. Pia, wengi wa wale ambao hali zao hazikuwaruhusu kufanya upainia msaidizi waliongeza utendaji wao. Hudhurio la Ukumbusho lilikuwa 66,364, karibu mara tatu ya wastani wa idadi ya wahubiri nchini Kenya.
Uganda: Ripoti ya mwezi wa Aprili inaonyesha vilele vipya katika sehemu nyingi za utendaji. Wahubiri 1,855 kati ya jumla ya wahubiri 5,438 walitumika wakiwa mapainia wasaidizi. Idadi hiyo ni karibu mara nne ya mapainia wasaidizi ambao wamewahi kutumika katika mwezi mmoja! Walitumia saa 165,358 katika huduma, wakafanya ziara za kurudia 80,741 na kuongoza mafunzo ya Biblia 15,222. Hudhurio la ukumbusho liliongezeka kufikia 21,393. Ni shangwe iliyoje kuwaona watu wa Yehova ‘wakishughulika sana na lile neno’!—Mdo. 18:5.