Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 31, 2011.
1. Kwa nini tushikamane na vikumbusho vya Yehova? (Zab. 119:60, 61) [w00 12/1 uku. 14 fu. 3]
2. Tunaweza kujifunza somo gani katika andiko la Zaburi 133:1-3? [w06 9/1 uku. 16 fu. 3]
3. Ni katika njia gani Yehova alikuwa ‘amemchunguza kabisa’ Daudi na ‘kupima kusafiri na kulala kwake akiwa amejinyoosha’? (Zab. 139:1, 3) [w06 9/1 uku. 16 fu. 6; w93 10/1 uku. 11 fu. 6]
4. Yehova “anawategemeza” au ‘kuwainua’ watumishi wake wanapokabili matatizo ya aina gani? (Zab. 145:14) [w04 1/15 uku. 17 fu. 11]
5. Ni mambo gani yanayomfanya mtu anayetajwa kwenye Methali 6:12-14 aonwe kuwa asiyefaa kitu? [w00 9/15 uku. 26 fu. 5-6]
6. Kwa nini mtu mwenye hekima ‘hukubali amri’? (Met. 10:8) [w01 7/15 uku. 26 fu. 1]
7. Wenye hekima hutofautianaje na wapumbavu wanapotukanwa au kuchambuliwa isivyofaa? (Met. 12:16) [w03 3/15 uku. 27 fu. 3-4]
8. Ni katika njia gani mtazamo unaofaa hutuwezesha kuwa na “karamu sikuzote”? (Met. 15:15) [w06 7/1 uku. 16 fu. 6]
9. Ni nini kinachohusika katika ‘kujipatia moyo’ na ni kwa njia gani anayefanya hivyo “anapenda nafsi yake mwenyewe”? (Met. 19:8) [w99 7/1 uku. 18 fu. 4; it-1-E uku. 1059 fu. 1]
10. Utambuzi au ufahamu unaweza kufaidije nyumba? (Met. 24:3) [w06 9/15 uku. 27 fu. 11; be uku. 31 fu. 6]