Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, zungumzia trakti Je, ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Vilevile, pamoja na broshua hiyo au badala yake, makutaniko yaweza kuamua kutoa yoyote kati ya broshua zilizokuwa toleo la Agosti 2011. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu au Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kinaweza kutolewa. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia gazeti la zamani au broshua yoyote inayomfaa.