Habari Kuu za Utumishi
Tanzania: Tulifurahi kuona mapainia wasaidizi 3,418 wakishiriki katika kampeni ya pekee wakati wa majira ya Ukumbusho mwezi wa Aprili. Hiyo ilikuwa asilimia 23 ya wahubiri waliotoa ripoti mwezi huo kutia ndani mapainia wa kawaida na wa pekee 1,566. Kwa sababu ya jitihada zao pamoja na bidii ya wahubiri wengine, mafunzo ya Biblia 26,304 yaliongozwa mwenzi wa Aprili. Hayo yalikuwa mafunzo 4,502 zaidi ya yale yaliyoongozwa mwaka uliotangulia.