Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 26, 2011.
1. Shauri lililo katika Methali 30:32 linaweza kutusaidiaje kuepuka kumkasirisha zaidi mtu ambaye huenda tumemuudhi? [w87 5/15 uku. 30 fu. 11]
2. Ni aina gani ya “kushangilia” ambayo haimridhishi mtu? (Mhu. 2:1) [g 4/06 uku. 6 fu. 1-2]
3. Ingawa watu fulani hufikiri kwamba maneno ya Sulemani yalirekodiwa katika Mhubiri 3:1-9 yanaunga mkono fundisho la majaliwa, mambo aliyosema katika Mhubiri 9:11 yanafunuaje ukweli wa mambo kwamba kila kitu maishani hakitokei kwa majaliwa? [w09 3/1 uku. 4 fu. 4]
4. Kuna hatari gani ya kuwa “mwadilifu kupita kiasi”? (Mhu. 7:16) [w10 10/15 uku. 9 fu. 8-9]
5. Andiko la Wimbo wa Sulemani 2:7 linaonyeshaje kwamba ni jambo la hekima kwa watu wanaofikiria kufunga ndoa kutochagua mwenzi haraka-haraka? [w06 11/15 uku. 19 fu. 1; w80 4/15 uku. 19 fu. 7]
6. Maneno, midomo ya Mshulami “inadondosha asali ya sega” na ‘asali na maziwa viko chini ya ulimi wake’ yanakazia nini? (Wim. 4:11) [w06 11/15 uku. 19 fu. 6]
7. Majina ya cheo “Mshauri wa Ajabu,” “Mungu Mwenye Nguvu,” na “Baba wa Milele,” yanafunua nini kuhusu sifa za Yesu na utawala wake katika ulimwengu mpya? (Isa. 9:6) [w91 4/15 uku. 5 fu. 7]
8. Ni nani leo wanaoweza kufananishwa na “taifa lenye kuasi imani” la Israeli, na ni nani atakayekuwa kama “fimbo” ya Yehova ya kuharibu taifa hilo? (Isa. 10:5, 6) [ip-1 uku. 145 fu. 4-5; uku. 153 fu. 20]
9. Kwa nini utabiri wa Isaya kwamba Babiloni “hatakaliwa kamwe” ni wenye kutokeza sana, na kutimizwa kwa utabiri huo kunatupa uhakikisho gani? (Isa. 13:19, 20) [g 11/07 uku. 9 fu. 4-5]
10. Ni wakati gani ambapo Yesu alipokea “ufunguo wa nyumba ya Daudi,” naye amekuwa akiutumia kufanya nini? (Isa. 22:22) [w09 1/15 uku. 31 fu. 2]