Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia kwenye ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia magazeti yoyote ya zamani au broshua inayomfaa. Februari: Wahubiri wanaweza kutoa mojawapo ya machapisho yafuatayo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, na Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia kwenye ziara ya kwanza. Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki na hakubali funzo la Biblia, mhubiri anaweza kumwachia magazeti yoyote ya zamani au broshua inayomfaa. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mwenye nyumba akipendezwa, mpe trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Unapowarudia watu waliohudhuria Ukumbusho au matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawashirikiani kwa ukawaida na kutaniko, kazia fikira kuanzisha mafunzo ukitumia kitabu Biblia Inafundisha.
◼ Kuanzia Februari, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Je, Unamfanya Yehova Kuwa Tumaini Lako?”
◼ Kuanzia gazeti la Mnara wa Mlinzi, toleo la watu wote la Februari 1, 2012, kutakuwa na mfululizo wenye kichwa “Masomo Yangu ya Biblia.” Mfululizo huo umekusudiwa kutumiwa na wazazi kuwafunza watoto wenye umri usiozidi miaka mitatu. Mfululuzo huo pamoja na mifululizo yenye kichwa “Wafundishe Watoto Wako” na “Kwa Ajili ya Vijana,” itaendelea kuchapishwa kwa zamu.