Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Mwezi wa Agosti kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 24,926 na ongezeko la asilimia 3 la idadi ya wahubiri katika mwaka wa utumishi wa 2011. Kwa wastani, mafunzo ya Biblia 40,396 yaliongozwa kila mwezi. Pia, kulikuwa na wastani wa funzo 1.1 la Biblia kwa kila mhubiri.
Tanzania: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 16,012 katika mwaka wa utumishi wa 2011. Hilo ni ongezeko la asilimia 3 kwa kulinganisha na mwaka wa utumishi uliotangulia. Pia, kulikuwa na kilele cha mapainia wasaidizi 3,418 katika mwezi wa Aprili, na kwa wastani kila mhubiri aliongoza funzo 1.1 la Biblia kila mwezi.
Uganda: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 5,580 walioshiriki huduma katika mwezi wa Agosti. Kulikuwa na ongezeko la asilimia 6 katika mwaka huo wa utumishi. Kwa wastani mafunzo ya Biblia 14,154 yaliongozwa kila mwezi katika mwaka huo wa utumishi, hilo likiwa ongezeko la asilimia 10. Ni shangwe iliyoje kushiriki katika mavuno hayo ya kiroho!—Luka 10:2.