Ratiba ya Juma Linaloanza Agosti 6
JUMA LINALOANZA AGOSTI 6
Wimbo 60 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
bt sura ya 24 ¶16-21 (Dak. 25)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Ezekieli 24-27 (Dak. 10)
Na. 1: Ezekieli 24:15-27 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Mungu Aliwaruhusu Waisraeli Wapigane Vita Chini ya Hali Zipi?—rs uku. 135 ¶5–uku. 136 ¶1 (Dak. 5)
Na. 3: Andiko la Ezekieli 18:20 Linapingana na Kutoka 20:5? (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Je Umejitayarisha kwa Ajili ya Muhula Mpya wa Shule? Mazungumzo. Waombe wasikilizaji wataje baadhi ya hali ngumu ambazo vijana Wakristo watakabili shuleni. Eleza jinsi wazazi wanavyoweza kutumia Fahirisi, vitabu Vijana Huuliza, na vifaa vingine vya kitheokrasi wakati wa ibada ya familia kuwatayarisha watoto wao ili waweze kushinda vishawishi na kueleza mambo wanayoamini. (1 Pet. 3:15) Chagua kichwa kimoja au viwili, na ueleze baadhi ya habari muhimu zinazopatikana katika machapisho yetu. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi walivyofaulu kutoa ushahidi walipokuwa shuleni.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Agosti. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 ili kuonyesha kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Kisha, kwa kutumia makala za kwanza za Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza, na vilevile andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu makala za kwanza za Amkeni! na, wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa. Tumia magazeti ya karibuni zaidi mliyo nayo kutanikoni.
Wimbo 97 na Sala