Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Agosti
“Leo, mara nyingi watu humwona Yesu kama alivyokuwa miaka elfu mbili iliyopita, yaani, kama mtoto katika hori au kama mtu aliyetundikwa kwenye mti wa mateso. Hata hivyo, unafikiri Yesu anafanya nini sasa? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho gazeti hili linasema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1, na mzungumzie habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na msome angalau andiko moja. Mtolee magazeti, kisha upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Watu wengi huamini miujiza. Wengine hutilia shaka. Je, unafikiri miujiza hutukia kweli? [Mruhusu ajibu.] Ahadi hii ya muujiza utakaotukia wakati ujao imewapa watu wengi tumaini. [Soma angalau andiko moja lililo katika ukurasa wa 9-10.] Gazeti hili linajibu vipingamizi vitatu ambavyo hutolewa mara nyingi kuhusu miujiza.”
Amkeni! Agosti
“Siku hizi, watu wengi huogopa kutembea wakiwa peke yao, hasa baada ya giza kuingia. Je, unafikiri kuna lolote linaloweza kufanywa ili kupunguza jeuri katika ulimwengu huu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mambo fulani ambayo sote tunaweza kufanya ili tuwe na amani zaidi pamoja na wengine. Pia linazungumzia jinsi unabii huu wenye kutia moyo utakavyotimizwa.” Soma Zaburi 72:7.