Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Katika mwezi wa Machi, asilimia 31 ya wahubiri wote walishiriki katika utumishi wa upainia kutia ndani upainia msaidizi. Kulikuwa na kilele kipya cha mapainia wa kawaida 2,816 na ongezeko la asilimia 4 la wahubiri katika mwezi wa Machi ikilinganishwa na wastani wa mwaka uliopita. Kwa kweli, mwezi wa Machi ulikuwa na ongezeko la utendaji.
Uganda: Ripoti yenye kusisimua ya Machi 2012 ilikuwa na vilele vifuatavyo ambavyo hatujawahi kuwa navyo: wahubiri 5,676, saa 171,391, magazeti 96,861, na ziara za kurudia 88,249. Kilele kipya cha mafunzo ya Biblia 16,347 kinawakilisha ongezeko la asilimia 15.5 ikilinganishwa na wastani wa mwaka uliopita. Ni shangwe iliyoje kujionea itikio kubwa sana katika mwezi huo wa pekee, kama inavyoonyeshwa na vilele hivyo!—Zab. 110:3.