Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 29, 2012. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa, ili ndugu na dada waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
1. Madhabahu ambayo Ezekieli aliona katika maono inafananisha nini? (Eze. 43:13-20) [Sept. 10, w07 8/1 uku. 10 fu. 4]
2. Nini kinachofananishwa na maji ya mto ambao Ezekieli aliona katika maono? (Eze. 47:1-5) [Sept. 17, w07 8/1 uku. 11 fu. 2]
3. Maneno “aliazimia moyoni mwake” yanafunua nini kuhusu maagizo ya kiroho ambayo Danieli alipokea alipokuwa kijana? (Dan. 1:8) [Sept. 24, dp uku. 33-34 fu. 7-9; uku. 36 fu. 16]
4. Nini kilichowakilishwa, au kufananishwa, na ule mti mrefu sana katika ndoto ya Nebukadneza? (Dan. 4:10, 11, 20-22) [Okt. 1, w07 9/1 uku. 18 fu. 5]
5. Andiko la Danieli 9:17-19 linatufundisha nini kuhusiana na sala? [Okt. 8, w07 9/1 uku. 20 fu. 5-6]
6. Ni agano gani ‘lililoendelea kutendeshwa kwa ajili ya wengi’ mpaka mwishoni mwa juma la 70 la miaka, au mwaka wa 36 W.K.? (Dan. 9:27) [Okt. 8, w07 9/1 uku. 20 fu. 4]
7. Tunaweza kukata kauli gani kutokana na maneno ambayo malaika alimwambia Danieli kwamba “mkuu wa ufalme wa Uajemi” alikuwa amesimama kumpinga? (Dan. 10:13) [Okt. 15, w11 9/1 uku. 8 fu. 1-2]
8. Ni unabii gani wa Biblia kumhusu Masihi ambao ulitimizwa kuhusiana na Danieli 11:20? [Okt. 15, dp uku. 232-233 fu. 5-6]
9. Kulingana na Hosea 4:11, ni hatari ipi moja ya kunywa pombe kupita kiasi? [Okt. 22, w10 1/1 uku. 4-5]
10. Andiko la Hosea 6:6 linatufundisha somo gani muhimu? [Okt. 22, w07 9/15 uku. 16 fu. 8; w05 11/15 uku. 24 fu. 11-12]