Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/12 uku. 7
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 12/12 uku. 7

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 31, 2012. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.

1. Unabii unaopatikana katika Yoeli 2:1-10, 28 kuhusu shambulio la wadudu umetimizwa kwa njia gani? [Nov. 5, w07 10/1 uku. 13 fu. 1]

2. Ni nani wanaotimiza andiko la Amosi 8:11, na kwa kuwa tuna chakula kingi cha kiroho, tunapaswa kujiuliza swali gani? [Nov. 12, jd uku. 60-61 fu. 9]

3. Ni jambo gani ambalo huenda lilichangia kimbelembele cha moyo wa Waedomu, na ni ukweli gani ambao hatupaswi kamwe kusahau? (Oba. 3, 4) [Nov. 19, w07 11/1 uku. 13 fu. 6]

4. Ni katika njia gani Yehova alijuta kuhusu msiba ambao alikuwa amesema ataleta juu ya wakaaji wa Ninawi? (Yona 3:8, 10) [Nov. 19, w07 11/1 uku. 14 fu. 13]

5. Kutembea katika jina la Mungu kutaimarishaje urafiki wetu pamoja naye? (Mika 4:5) [Nov. 26, jd uku. 88 fu. 12]

6. Utimizo wa unabii unaopatikana katika Nahumu 2:6-10 unatupa uhakikisho gani? [Des. 3, w07 11/15 uku. 9 fu. 2; w88 2/15 uku. 28 fu. 8]

7. Andiko la Hagai 1:6, linamaanisha nini, na tunapaswa kutilia maanani somo gani? [Des. 10, w06 4/15 uku. 22 fu. 12-15]

8. Tunawezaje kutumia shauri linalopatikana kwenye Zekaria 7:10 kwamba ‘tusipangiane jambo lolote baya mioyoni mwetu’? [Des. 17, jd uku. 113 fu. 6; w07 12/1 uku. 11 fu. 2]

9. Ni kwa nini maneno ya Zekaria 4:6, 7 ni yenye kufariji kwa waabudu wa Yehova leo? [Des. 17, w07 12/1 uku. 10 fu. 7]

10. Kulingana na andiko la Malaki 3:16, kwa nini hatupaswi kamwe kudhoofisha azimio letu la kudumisha utimilifu wetu kwa Mungu? [Des. 31, w07 12/15 uku. 29 fu. 3]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki