Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 31
JUMA LINALOANZA DESEMBA 31
Wimbo 60 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 3 ¶7-12 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Malaki 1-4 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: “Mfululizo Mpya Utakaokuwa Katika Mnara wa Mlinzi.” Hotuba. Tumia mapendekezo yaliyo katika ukurasa wa 8 kupanga onyesho la jinsi tunavyoweza kutumia magazeti kuanzisha funzo la Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Januari. Ikiwa magazeti ya mwezi wa Januari hayapatikani kutanikoni, eleza jinsi mfululizo huo mpya utakavyotumiwa kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 10: Tunajifunza Nini? Mazungumzo. Omba wasikilizaji wasome Luka 10:38-42. Zungumzia jinsi simulizi hilo linavyoweza kutusaidia katika huduma.
Dak. 10: Toleo la Machapisho la Mwezi wa Januari na Februari. Mazungumzo. Zungumzia baadhi ya mambo yenye kuvutia yaliyomo katika machapisho yatakayotolewa na upange kuwe na maonyesho mawili.
Wimbo 134 na Sala