Tovuti Yetu Rasmi—Itumie Kumhubiria Mtu Anayezungumza Lugha Tofauti
Mwonyeshe Tovuti Yetu: Mwonyeshe jinsi ya kutumia orodha ya “Lugha ya Tovuti” ili aweze kuona Tovuti hiyo katika lugha yake. (Katika baadhi ya lugha, ni sehemu fulani tu ya Tovuti hiyo inayopatikana.)
Mwonyeshe Ukurasa wa Tovuti Hiyo Katika Lugha Yake: Fungua ukurasa mmoja wa machapisho yetu, kama vile kitabu Biblia Inafundisha au trakti Kujua Ukweli. Chagua lugha ya mwenye nyumba kwenye orodha ya “Soma Katika.”
Mruhusu Asikilize Makala Fulani: Tafuta makala ambayo inaweza kusikilizwa katika lugha ya mtu unayemhubiria, na umchezee rekodi ya makala hiyo. Ikiwa unajifunza lugha nyingine, boresha uwezo wako kwa kusikiliza rekodi ya chapisho katika lugha hiyo unapoisoma.—Nenda kwenye “Machapisho/Vitabu na Broshua” au “Machapisho/Magazeti.”
Wahubirie Viziwi: Ukimpata mtu ambaye ni kiziwi, mwonyeshe video ya lugha ya ishara ya sura ya Biblia, kitabu, broshua, au trakti.—Nenda kwenye “Machapisho/Lugha ya Ishara.”
[Picha katika ukurasa wa 6]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
Jaribu Kuitumia
1 Bonyeza ▸ ili usikilize rekodi ya sauti uliyochagua (iwapo inapatikana katika lugha yako) au mojawapo ya vitufe vya “Machaguo ya Upakuaji” ili kupakua chapisho hilo.
2 Chagua lugha nyingine kutoka kwenye orodha ya “Soma Katika” ili kuonyesha ukurasa huu katika lugha hiyo.
3 Bonyeza “Inayofuata” au kiunganishi katika “Yaliyomo” ili usome makala au sura nyingine.