Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Januari
“Tungependa kujua maoni yako. Unafikiri Mungu anaitwa nani? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi gazeti hili linavyosema.” Mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na umwonyeshe makala iliyo kwenye ukurasa wa nyuma. Zungumzieni habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti na upange kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Watu wengi wamekuwa wakizungumza kuhusu mwisho wa ulimwengu. Je, unafikiri tunapaswa kuogopa mwisho wa ulimwengu? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na andiko hili, kutakuwa na watu watakaookoka mwisho wa ulimwengu. [Soma 1 Yohana 2:17.] Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia ya maswali manne ambayo kwa kawaida watu huuliza kuhusu mwisho wa ulimwengu.”
Amkeni! Januari
“Leo tunatembelea familia tukiwa na ujumbe muhimu ambao tungependa kushiriki pamoja nao. Je, unafikiri ni jambo la muhimu kutumia maneno haya ya Yesu? [Soma Matendo 20:35b. Kisha mruhusu ajibu.] Kuwafundisha watoto kuwa wakarimu kunaweza kuwa jambo gumu sana katika ulimwengu ambao watu wengi huwa na mtazamo wa kujifikiria wenyewe tu. Makala hii inataja baadhi ya njia ambazo wazazi wanaweza kuwazoeza watoto wao wawajali wengine.”