Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza ya Mwezi wa Januari
“Watu fulani wanaamini kwamba Biblia ni kitabu cha unabii kinachotegemeka. Wengine wanahisi kuwa kina matabiri yasiyo ya hakika yanayoweza kufasiriwa kwa njia mbalimbali. Una maoni gani?” Mruhusu ajibu. Kisha mpe mwenye nyumba gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, na mpitie pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo katika ukurasa wa 16 na angalau msome mojawapo ya maandiko yanayotajwa. Mwachie gazeti na upange kumrudia ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Tunaweza kujifunza mambo mengi kutoka kwa wanaume na wanawake mashuhuri walioishi zamani. Je, unakubali jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili linamrejelea mtu fulani mashuhuri ambaye ndiye pekee anayetajwa na Biblia kuwa ‘rafiki ya Mungu.’ [Soma Yakobo 2:23.] Gazeti hili linaeleza kwa nini Mungu alimwona mwanamume huyo kuwa rafiki yake na linazungumzia mambo tunayoweza kujifunza kutoka kwa Abrahamu.”
Amkeni! Januari
“Kutoa rushwa, au hongo, na aina nyingine ya ukosefu wa unyoofu ni mambo ya kawaida katika ulimwengu wa biashara. Watu wengine wanaona kwamba mtu hawezi kuwa mnyoofu kabisa katika biashara na afaulu. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Ona methali hii inayokuchochea ufikiri. [Soma Methali 20:17.] Gazeti hili linaeleza kwa nini ni muhimu kuwa wanyoofu.”