Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Januari
“Watu wengi wana maoni yanayotofautiana kuhusu Mungu. Baadhi yao hufikiri Mungu ni nguvu isiyoeleweka. Ilhali wengine humwona kuwa Baba wa mbinguni mwenye upendo. Wewe unafikiri Mungu yukoje?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, na mzungumzie pamoja habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau andiko moja lililoonyeshwa. Mwachie magazeti, na ufanye mpango wa kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Tunawatembelea kifupi ili kuzungumzia jambo linalotupata sisi sote, yaani kufiwa na wapendwa wetu. Je, utakubaliana nami kwamba kufiwa na rafiki wa karibu au mtu wa ukoo ni mojawapo ya mambo magumu zaidi kukabiliana nayo? [Mruhusu ajibu.] Andiko hili limewafariji watu wengi. [Soma Isaya 25:8.] Gazeti hili linazungumzia ahadi ya Biblia yenye kutia moyo ya kuondoa kifo na kuwafufua wapendwa wetu.”
Amkeni Januari
“Je, unakubali kwamba leo familia zinakabili mahangaiko mengi sana? [Mruhusu ajibu.] Methali hii ya Biblia inatuambia jambo ambalo familia zinaweza kufanya ili ziwe imara. [Soma Methali 24:3.] Watu wengi wametambua kwamba Biblia ni chanzo kinachotegemeka cha hekima. Gazeti hili linazungumzia kuhusu Tovuti ya kipekee inayotegemea Biblia, yenye habari zinazopatikana bila malipo ambazo zimekusudiwa kusaidia familia.”