Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Je, unafikiri ulimwengu utakuwa bora ikiwa kila mtu atatumia kanuni hii maishani? [Soma Waebrania 13:18, na umruhusu ajibu.] Biblia inatutia moyo sote tuwe wanyoofu katika kila jambo. Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi unyoofu ulivyo muhimu maishani mwetu.”
Amkeni Januari
“Nimekuletea gazeti la Amkeni! la mwezi huu. [Mpe magazeti.] Ona swali kwenye ukurasa wa 2 na majibu ambayo kwa kawaida watu hutoa. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia kanuni kadhaa za Biblia ambazo zinaweza kutusaidia kuboresha mtazamo wetu maishani.”