Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kuondoa tatizo moja hapa ulimwenguni, ungeondoa tatizo lipi? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, hivi karibuni Mungu ataondoa tatizo hilo na mengine mengi. [Chagua andiko utakalosoma, kama vile Danieli 2:44; Methali 2:21, 22; Mathayo 7:21-23; au 2 Petro 3:7.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi Mungu atakavyofanya mabadiliko hayo hapa duniani na ni lini atafanya hivyo.”
Amkeni Mei
“Je, unafikiri kwamba tutawahi kuishi katika ulimwengu ambao watu wote watakuwa na nyumba nzuri na bila umaskini? [Mruhusu ajibu.] Tafadhali ona yale ambayo Mungu amewaahidi wanadamu kuhusu jambo hilo. [Soma Isaya 65:21, 22.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia jinsi ambavyo Mungu atakavyotimiza ahadi zake na jinsi tunavyoweza kunufaika.”