Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Februari 25, 2013. Tarehe ambayo kila sehemu itazungumziwa imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wanapofanya matayarisho kwa ajili ya shule kila juma.
1. Kwa nini Yesu alisema kwamba “wale wanaoomboleza” wangekuwa na furaha? (Mt. 5:4) [Jan. 7, w09 2/15 uku. 6 fu. 6]
2. Katika sala ya kielelezo aliyowafundisha wanafunzi wake, Yesu alimaanisha nini aliposema: “Usituingize katika jaribu”? (Mt. 6:13) [Jan. 7, w04 2/1 uku. 16 fu. 13]
3. Kwa nini Yesu alisema kwamba wanafunzi wake hawangemaliza mzunguko wao wa kuhubiri “mpaka Mwana wa binadamu atakapofika”? (Mt. 10:23) [Jan. 14, w10 9/15 uku. 10 fu. 12; w87 8/1 uku. 8 fu. 6]
4. Mfano wa Yesu wa mbegu ya haradali unakazia mambo gani mawili? (Mt. 13:31, 32) [Jan. 21, w08 7/15 uku. 17-18 fu. 3-8]
5. Yesu alikuwa akifundisha somo gani aliposema: “Msipogeuka na kuwa kama watoto wachanga, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”? (Mt. 18:3) [Jan. 28, w07 2/1 uku. 9-10 fu. 3-4]
6. Maneno ya Yesu “wewe mwenyewe umesema” yanamaanisha nini? (Mt. 26:63, 64) [Feb. 11, w11 6/1 uku. 18]
7. Kwa nini Yesu anaitwa “Bwana hata wa sabato”? (Marko 2:28) [Feb. 18, w08 2/15 uku. 28 fu. 7]
8. Kama tunavyosoma katika Marko 3:31-35, kwa nini Yesu aliitikia kwa njia hiyo kuelekea mama yake na ndugu zake, na hilo linatufundisha nini? [Feb. 18, w08 2/15 uku. 29 fu. 5]
9. Kama tunavyosoma katika Marko 8:22-25, huenda ni kwa nini Yesu alimponya mtu aliyekuwa kipofu kwa hatua mbili, na tunajifunza nini kutokana na jambo hilo? [Feb. 25, w00 2/15 uku. 17 fu. 7]
10. Tunajifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyoitikia kemeo la Petro kwenye Marko 8:32-34? [Feb. 25, w08 2/15 uku. 29 fu. 6]