Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 29, 2013. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
1. Ni kikumbusho gani kuhusu ndoa kilichoandikwa kwenye Marko 10:6-9 ambacho Yesu alitoa? [Mac. 4, w08 2/15 uku. 30 fu. 8]
2. Kumtumikia Yehova kwa nafsi yote kunamaanisha nini? (Marko 12:30) [Mac. 4, w97 10/15 uku. 13 fu. 4]
3. “Maumivu ya taabu” yanayotajwa kwenye Marko 13:8 ni nini? [Mac. 11, w08 3/15 uku. 12 fu. 2]
4. Ni vyanzo gani vya habari ambavyo Luka alichunguza alipokuwa akikusanya masimulizi yake ya Injili? (Luka 1:3) [Mac. 18, w09 3/15 uku. 32 fu. 4]
5. Kwa kuwa Shetani hutafuta ‘wakati unaofaa’ wa kujaribu utimilifu wetu, tunapaswa kufanya nini? (Luka 4:13) [Mac. 25, w11 1/15 uku. 23 fu. 10]
6. Tunafaa kuyatumiaje maneno yanayopatikana kwenye Luka 6:27, 28? [Mac. 25, w08 5/15 uku. 8 fu. 4]
7. Yesu angewezaje kumsamehe mwanamke mwenye dhambi kabla ya kufa na kutoa dhabihu ya fidia? (Luka 7:37, 48) [Apr. 1, w10 8/15 uku. 6-7]
8. Ni katika maana gani wafuasi wa Kristo wanapaswa ‘kuwachukia’ watu wa ukoo? (Luka 14:26) [Apr. 15, w08 3/15 uku. 32 fu. 1; w92 7/15 uku. 9 fu. 3-5]
9. “Ishara [zitakazokuwa] katika jua, na mwezi na nyota” zitakuwa na matokeo gani kwa wanadamu? (Luka 21:25) [Apr. 22, w97 4/1 uku. 15 fu. 8-9]
10. Tunawezaje kuiga njia ya Yesu ya kusali tunapopatwa na majaribu ambayo ni makali zaidi? (Luka 22:44) [Apr. 29, w07 8/1 uku. 6 fu. 2]