Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 27
JUMA LINALOANZA MEI 27
Wimbo 6 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 10 ¶1-7 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yohana 12-16 (Dak. 10)
Na. 1: Yohana 12:20-36 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Thamani ya Dhabihu ya Yesu Ilitumiwa kwa Faida ya Nani Kwanza, na kwa Kusudi Gani?—rs uku. 80 ¶2-3 (Dak. 5)
Na. 3: Kwa Nini Ni Jambo Linalofaa Kwamba Yehova Anaitwa “Mungu Anayetoa Amani”?—Rom. 15:33 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Kuanzisha Funzo la Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza. Hotuba. Tumia ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi kupanga onyesho la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Juni. Watie moyo wote washiriki katika utumishi.
Dak. 15: Kutia Maji Mbegu Tunazopanda. (1 Kor. 3:6-9) Mazungumzo yanayotegemea maswali yafuatayo: (1) Ni mambo gani unayofurahia unapofanya ziara za kurudia? (2) Wengine hukabili hali gani ngumu wanapofanya ziara za kurudia? (3) Tunaweza kukabilianaje na hali hizo? (4) Inapokuwa vigumu kwetu kufanya ziara za kurudia, tunaweza kupata wapi msaada? (5) Unafanya nini ili ukumbuke kumrudia mtu aliyependezwa, jambo mlilozungumzia, chapisho ulilomwachia, na mambo mengine? (6) Unajitayarishaje kwa ajili ya ziara za kurudia? (7) Kwa nini ni vizuri kutenga wakati kila juma ili kufanya ziara za kurudia?
Dak. 10: “Tumia Video Unapofundisha.” Mazungumzo. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi walivyonufaika walipotazama video zetu kabla ya kuwa Mashahidi. Mahali ambapo video hazipatikani onyesha jinsi tunavyoweza kutumia picha katika kitabu Biblia Inafundisha na “Upendo wa Mungu” ili kukazia mafundisho muhimu katika akili za wanafunzi wa Biblia.
Wimbo 101 na Sala