Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 3
JUMA LINALOANZA JUNI 3
Wimbo 68 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 10 ¶8-13 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yohana 17-21 (Dak. 10)
Na. 1: Yohana 21:15-25 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kwa Nini Hatupaswi ‘Kuufuata Umati’?—Kut. 23:2; Met. 1:10 (Dak. 5)
Na. 3: Ni Nani Wengine Kando na Wakristo Watiwa-Mafuta Wanaofaidika na Dhabihu ya Yesu?—rs uku. 81 ¶1-3 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Juni. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 kuonyesha kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Halafu, kwa kutumia habari kuu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza na kisha watoe mapendekezo ya andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu gazeti la Amkeni! na wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja kutoka katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga kuwe na onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa ukitumia magazeti ya karibuni zaidi yanayopatikana kutanikoni na Huduma Yetu ya Ufalme yenye mapendekezo ya jinsi ya kuyatoa magazeti hayo.
Dak. 10: Kwa Nini Sisi Huripoti Utumishi Wetu wa Shambani? Hotuba itolewe na mwandishi ikitegemea kitabu Tengenezo, ukurasa wa 88, fungu la 2, hadi ukurasa wa 90, fungu la 2.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Wimbo 107 na Sala