Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 24, 2013. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
1. Katika andiko la Yohana 3:14, 15, Yesu alimaanisha nini aliposema: “Kama vile Musa alivyoinua nyoka nyikani, ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa”? [Mei 6, it-1 uku. 505]
2. Ni wakati gani ambapo wafuasi wa Kristo hupokea uzima ndani yao wenyewe, au hupata uhai kamili? (Yoh. 6:53) [Mei 13, w03 9/15 uku. 31 fu. 3]
3. Toa mfano unaoonyesha jinsi Yesu alivyomfunua Baba yake kwa wanadamu wasio wakamilifu. (Yoh. 8:28) [Mei 20, w11 4/1 uku. 7 fu. 2]
4. Tunajifunza nini kutokana na kitendo cha Yesu cha ‘kutokwa na machozi’ baada ya kifo cha Lazaro rafiki yake? (Yoh. 11:35) [Mei 20, w08 5/1 uku. 24 fu. 3-5]
5. Tunajifunza somo gani muhimu kutokana na kitendo cha Yesu cha kuwaosha miguu wanafunzi wake? (Yoh. 13:4, 5) [Mei 27, w99 3/1 uku. 31 fu. 1]
6. Roho ya Mungu inawezaje kutupatia mwongozo ulio hakika? (Yoh. 14:26) [Mei 27, w11 12/15 uku. 15 fu. 9]
7. Katika andiko la Yohana 21:15, ni nani wanaorejezewa kama “hawa,” na ni somo gani tunaloweza kujifunza? [Juni 3, w08 4/15 uku. 32 fu. 12]
8. Kulingana na Matendo 2:44-47 na Matendo 4:34, 35, Wakristo wanafaa kuiga roho ya aina gani? [Juni 10, w08 5/15 uku. 30 fu. 5]
9. Katika simulizi linalopatikana kwenye Matendo 7:59, je, Stefano alikuwa akisali kwa Yesu? [Juni 17, w08 5/15 uku. 31 fu. 2]
10. Tunaweza kuigaje kielelezo kizuri cha Barnaba, na tutafaidikaje tukifanya hivyo? (Mdo. 9:26, 27) [Juni 24, bt uku. 65 fu. 19]