Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 24
JUMA LINALOANZA JUNI 24
Wimbo 123 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 11 ¶1-8 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Matendo 8-10 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 20)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: “Zungumzia Jambo Moja, Lakini Mwachie Magazeti Mawili.” Hotuba. Kwa kutumia pendekezo lililo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na onyesho la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Julai. Onyesho hilo lifanywe baada ya hotuba.
Dak. 10: Kazi Yetu Si ya Bure. (Ebr. 6:10) Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka—2013, ukurasa wa 113-115. Waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza.
Dak. 10: Toleo la Machapisho la Mwezi wa Julai na Agosti. Mazungumzo. Zungumzia kifupi mambo yaliyomo katika broshua zitakazotolewa. Panga kuwe na onyesho la jinsi broshua mbili kati ya hizo zinavyoweza kutolewa. Onyesho moja linapaswa kuwa la broshua Habari Njema. Onyesho hilo linapaswa kufanywa kwa kutumia pendekezo lililo katika ukurasa wa 8 au mojawapo ya mapendekezo yaliyo katika ukurasa wa 6 na 7 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2013.
Wimbo 129 na Sala