Ratiba ya Juma Linaloanza Julai 15
JUMA LINALOANZA JULAI 15
Wimbo 48 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 12 ¶1-7 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Matendo 18-21 (Dak. 10)
Na. 1: Matendo 20:17-38 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Je, Kristo Atatokea Akionekana kwa Macho Juu ya Wingu, Kisha Awachukue Wakristo Waaminifu Waende Mbinguni Huku Ulimwengu Ukitazama?—rs uku. 111 ¶2–uku. 112 ¶1 (Dak. 5)
Na. 3: Tunaweza Kuonyeshaje Kwamba Tunakaza Akili Juu ya Roho?—Rom. 8:6 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Ufikie Moyo wa Mwanafunzi Wako. (Luka 24:32) Mazungumzo yanayotegemea maswali haya: (1) Unapoongoza funzo la Biblia, kwa nini ni muhimu kukazia (a) upendo na hekima ya Yehova? (b) umuhimu wa kutumia kanuni za Biblia? (c) uhitaji wa kutafuta mwelekezo wa Yehova nyakati zote kabla ya kufanya uamuzi? (2) Kumuuliza mwanafunzi wako maswali yafuatayo kutakusaidiaje kutambua ikiwa unaufikia moyo wake? (a) Je, unahisi jambo hili linapatana na akili? (b) Je, unafikiri jambo hili linapatana na upendo wa Mungu? (c) Kuna faida gani ya kutumia shauri hili?
Dak. 20: “Ndugu Vijana, Je, Mnajitahidi Kufikia Mapendeleo?” Maswali na majibu. Mhoji kwa ufupi mzee au mtumishi wa huduma ambaye alijitahidi kufikia mapendeleo akiwa kijana. Alipokea migawo na mazoezi gani kabla ya kuwekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma? Wengine kutanikoni walimsaidiaje kufanya maendeleo ya kiroho? Amefurahia baraka gani kutokana na kujitahidi kufikia mapendeleo?
Wimbo 85 na Sala