Matangazo
◼ Toleo la machapisho la mwezi wa Agosti: Habari Njema Kutoka kwa Mungu! au mojawapo ya broshua zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je, Kweli Mungu Anatujali?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, au yoyote kati ya broshua zenye kurasa 32 zinazopatikana katika kutaniko lenu. Septemba na Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Novemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? au mojawapo ya trakti zifuatazo: Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?, au Je, Ungependa Kujua Ukweli?
◼ Kuanzia juma linaloanza Oktoba 28, 2013, tutaanza kujifunza broshua yenye kichwa Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? katika Funzo la Biblia la Kutaniko. Baada ya kumaliza kujifunza broshua hiyo, tutajifunza kitabu Mkaribie Yehova kuanzia juma linaloanza Januari 6, 2014. Makutaniko yanayohitaji machapisho hayo yanapaswa kuyaagiza katika ombi lao la machapisho linalofuata.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa ‘Habari Njema kwa Kila Taifa, Kabila na Lugha.’ Katika makutaniko ambayo hotuba hiyo ilitolewa, hotuba yenye kichwa “Jinsi Ambavyo Upendo na Imani Huushinda Ulimwengu” itatolewa.