Ratiba ya Juma Linaloanza Oktoba 7
JUMA LINALOANZA OKTOBA 7
Wimbo 92 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 15 ¶1-6, sanduku kwenye uku. 184 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Waefeso 1-6 (Dak. 10)
Na. 1: Waefeso 4:1-16 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kinachomaanishwa na Kuutafuta Kwanza Uadilifu wa Mungu—Mt. 6:33 (Dak. 5)
Na. 3: Je, Ni Kweli Kwamba Kuna Wema Katika Dini Zote?—rs uku. 60 ¶1-3 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa Oktoba. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 kueleza kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Halafu, kwa kutumia habari kuu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi ambalo watauliza na kisha watoe mapendekezo ya andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu gazeti la Amkeni! na wakati ukiruhusu, kuhusu makala nyingine moja kutoka katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga kuwe na onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Wanaofanya Kazi kwa Bidii. (1 The. 5:12, 13) Wahoji wazee wawili. Wana migawo gani kutanikoni na wanashughulikia migawo gani mingine ya kitheokrasi? Wanafanya nini ili wafaulu kushughulikia migawo yao kutia ndani kazi za kimwili na majukumu ya kifamilia? Wanafanya nini ili kutanguliza huduma? Familia zao zimewasaidiaje?
Wimbo 123 na Sala