Habari Kuu za Utumishi
Uganda: Tunafurahi kuwajulisha kwamba katika mwezi wa Machi kulikuwa na vilele sita vipya ambavyo havijawahi kufikiwa. Kulikuwa na jumla ya wahubiri 6,156 kutia ndani mapainia wa kawaida 762 waliotoa ripoti ya saa 183,806, magazeti 127,914, ziara za kurudia 93,221, na mafunzo ya Biblia 17,048. Kwa kuongezea, kulikuwa na jumla ya mapainia wasaidizi 1,847. Ni jambo lenye kutia moyo kuona wengi ‘wakifanya kazi kwa bidii na kujikaza wenyewe’ katika ibada safi.—1 Tim. 4:10.