Matangazo
◼ Machapisho yatakayotolewa mwezi wa Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? au mojawapo kati ya trakti zifuatazo: Je, Ungependa Kujua Ukweli?, Kuteseka Kote Kutaisha Karibuni!, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, au Yehova—Yeye Ni Nani?, na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Julai: Habari Njema Kutoka kwa Mungu! au yoyote kati ya broshua zifuatazo: Msikilize Mungu, Msikilize Mungu Uishi Milele, na Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! Agosti: Usambazaji wa trakti mpya inayotangaza Tovuti ya jw.org. Katika eneo ambalo trakti hiyo haitafaa, broshua ya Habari Njema Kutoka kwa Mungu! au yoyote kati ya broshua zifuatazo: Msikilize Mungu, Msikilize Mungu Uishi Milele, na Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! zinaweza kutolewa. Septemba na Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
◼ Kuanzia mwishoni mwa mwaka wa utumishi wa 2014, Shule ya Utumishi wa Painia itafanywa kwa siku sita, kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi.
◼ Ratiba ya mikutano ya juma moja kabla ya kusanyiko lenu la eneo, inapaswa kurekebishwa ili kuzungumzia mashauri na vikumbusho vinavyopatikana kwenye nyongeza iliyo katika toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme na barua kwa makutaniko yote ya Agosti 3, 2013, inayohusu kudumisha usalama tunapohudhuria programu za kiroho. Mwezi mmoja au miwili baada ya kusanyiko, mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kutaniko ili kupitia mambo hususa ambayo wahubiri wamejifunza kusanyikoni yatakayowasaidia katika utumishi wa shambani.