Ratiba ya Juma la Novemba 3
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 3
Wimbo 79 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 15 ¶11-19 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 14-18 (Dak. 10)
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 15:16–16:8 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Kwa Nini Tunapaswa Kutambua Kwamba Kuna Dhambi—rs uku. 56 ¶1–uku. 57 ¶1 (Dak. 5)
Na. 3: Tunahitaji Kukaa Macho Kuelekea Ishara za Siku za Mwisho—td 30B (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Wasaidie Watoto Wajitayarishe kwa Ajili ya Utumishi. Mazungumzo. Onyesha video yenye kichwa Uwe Rafiki ya Yehova—Twende Tukahubiri. (Nenda kwenye Tovuti ya jw.org/sw, na angalia chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > WATOTO.) Waulize watoto: Ni nani kati yenu ana mkoba wa utumishi? Umeweka nini kwenye mkoba wako? Sofia aliweka nini kwanza kwenye mkoba wake? Alihitaji nini kingine? Baada ya kupanga mkoba wake, alienda kufanya jambo gani muhimu pamoja na mama yake? Panga kuwe na onyesho la mtoto anayetoa gazeti. Ikiwa video haipatikani, badili maswali hayo ili yafaane na hali za watoto katika kutaniko lenu.
Dak. 10: Jinsi Wengine Wanavyolihubiri Neno kwa Hisi ya Uharaka. Mzee awahoji wahubiri wawili au watatu ambao wamechukua hatua zinazofaa kurekebisha ratiba zao ili kuongeza utendaji wao katika huduma au kufanya upainia. Malizia kwa kupitia mipango ya utumishi wa shambani ya kutaniko, na uwatie moyo wote wachukue hatua zinazofaa ili washiriki kikamili katika kazi ya kuhubiri.
Dak. 10: Pitia Utendaji wa Kutaniko wa Mwezi wa Oktoba. Mazungumzo. Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi makala za karibuni zenye kichwa “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma” zilivyowasaidia kuboresha utumishi wao. Malizia kwa kuwatia moyo wote waendelee kuhubiri kwa hisi ya uharaka wakitumia mapendekezo yaliyo kwenye makala hizo.
Wimbo 100 na Sala