Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/14 kur. 2-3
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 12/14 kur. 2-3

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

1. Wahubiri wanaoongoza mafunzo ya Biblia wana jukumu gani?

1 Hakuna mtu anayeweza kumtumikia Mungu isipokuwa Yehova “amvute.” (Yoh. 6:44) Hata hivyo, wahubiri wanaoongoza mafunzo ya Biblia wanapaswa kutimiza sehemu yao kwa kuwasaidia watu wamkaribie Baba yao wa mbinguni. (Yak. 4:8) Jambo hilo linahitaji matayarisho. Ikiwa tunataka kuwasaidia wanafunzi waelewe habari tunayojifunza na kufanya maendeleo, haitoshi tu kusoma mafungu na kuuliza maswali yaliyochapishwa.

2. Wahubiri wanapaswa kutimiza nini wanapoongoza funzo la Biblia?

2 Ili kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo wahubiri wanapaswa kuwasaidia wanafunzi (1) waelewe Biblia inafundisha nini, (2) wakubali yale ambayo Biblia inafundisha, na (3) watumie mambo wanayojifunza kutoka katika Biblia. (Yoh. 3:16; 17:3; Yak. 2:26) Huenda ikachukua miezi kadhaa kumsaidia mtu afikie hatua hizo. Hata hivyo, kila moja ya hatua hizo itamsaidia ajenge uhusiano wake pamoja na Yehova na kujiweka wakfu kwake.

3. Kwa nini walimu stadi huuliza maswali ya maoni?

3 Mwanafunzi wa Biblia ana Maoni Gani?: Ili kutambua ikiwa mwanafunzi anaelewa na kukubali mambo anayojifunza, epuka kutawala mazungumzo, badala yake mtie moyo mwanafunzi ajieleze. (Yak. 1:19) Je, anaelewa yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu habari mnayozungumzia? Je, anaweza kuyaeleza kwa maneno yake mwenyewe? Anahisije kuhusu mambo ambayo amejifunza? Je, anaamini kwamba yale ambayo Biblia inafundisha yanapatana na akili? (1 The. 2:13) Je, anaelewa kwamba mambo anayojifunza yanapaswa kubadili jinsi anavyoishi? (Kol. 3:10) Ili kujua mambo hayo, tunapaswa kumuuliza maswali ya maoni kwa busara, kisha tumsikilize.—Mt. 16:13-16.

4. Tunapaswa kufanya nini ikiwa ni vigumu kwa mwanafunzi kuelewa au kutumia mambo anayojifunza katika Biblia?

4 Mara nyingi inachukua muda kwa mtu kubadili mazoea na njia yake ya kufikiri. (2 Kor. 10:5) Vipi ikiwa mwanafunzi wetu hakubali au hatumii mambo anayojifunza? Tunahitaji kuwa na subira ili kuruhusu Neno la Mungu na roho takatifu ifanye kazi katika moyo wa mwanafunzi. (1 Kor. 3:6, 7; Ebr. 4:12) Ikiwa ni vigumu kwa mwanafunzi kuelewa au kutumia fundisho fulani la Biblia, mara nyingi ni afadhali kuendelea na somo lingine badala ya kumshinikiza. Tunapoendelea kumfundisha Biblia kwa subira na upendo, huenda baadaye akachochewa kufanya mabadiliko yanayohitajika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki