Ratiba ya Juma Linaloanza Desemba 15
JUMA LINALOANZA DESEMBA 15
Wimbo 1 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 17 ¶9-16 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 6-8 (Dak. 10)
Na. 1: Yoshua 8:18-29 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Ni Nini Kinachoonyesha Kwamba Mtu Ana Roho Takatifu?—rs uku. 243 ¶3–uku. 244 ¶2 (Dak. 5)
Na. 3: Lazima Muungano wa Ndoa Uheshimiwe—td 26A (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Toa “mambo mema” kutoka katika hazina njema tuliyokabidhiwa.—Mt. 12:35a.
Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, panga kuwe na onyesho lenye sehemu mbili linaloonyesha mhubiri na mwanafunzi wakizungumzia fungu la 8 katika sura ya 15 ya kitabu Biblia Inafundisha. Katika sehemu ya kwanza, mhubiri anaongea sana. Katika sehemu ya pili, mhubiri anatumia maswali ili kutambua maoni ya mwanafunzi.
Dak. 15: Kifaa Kitakachokusaidia Kujitayarisha Kuongoza Mafunzo ya Biblia. Mazungumzo. Waeleze wasikilizaji kuhusu sehemu yenye kichwa “Biblia Inafundisha Nini?” iliyo katika Tovuti ya jw.org/sw. (Tazama chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA.) Zungumzia jinsi habari hiyo inavyoweza kutusaidia kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo pamoja vijana na hata watu wazima. Maswali yaliyo katika sehemu hiyo yanawezaje kutusaidia kufikia mioyo ya wanafunzi wetu? Panga kuwe na onyesho la mhubiri anayejizungumzia akitumia sehemu hiyo ili kumsaidia kutafakari kuhusu uhitaji wa mwanafunzi wake na kutayarisha maswali kwa ustadi. Malizia kwa kuwatia moyo wasikilizaji wawe walimu bora kwa kujitahidi kuifikia mioyo ya wanafunzi wao na wafanye hivyo kwa kutumia mambo mema tuliyonayo ili kuwasaidia wengine.—Met. 20:5.
Wimbo 99 na Sala