Matangazo
◼ Machapisho yatakayotolewa mwezi wa Machi na Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mei na Juni: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Au mojawapo ya trakti zifuatazo: Je, Kuteseka Kutaisha?, Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?, Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?, na Ni Nini Siri ya Kuwa na Familia Yenye Furaha?
◼ Ukumbusho utafanyika Ijumaa, Aprili 3, 2015. Ikiwa kwa kawaida kutaniko lenu hufanya mikutano siku ya Ijumaa, mikutano hiyo inaweza kufanywa siku nyingine katika juma hilo inapowezekana. Ikiwa haitawezekana kufanya Mkutano wa Utumishi juma hilo, mratibu wa baraza la wazee anaweza kufanya marekebisho katika ratiba ili kwamba habari fulani zinazohusu kutaniko lenu zizungumziwe ndani ya mwezi huo.