Habari Kuu za Utumishi
Uganda: Ripoti ya utumishi wa shambani ya mwezi wa Agosti pamoja na ripoti ya mwisho wa mwaka wa utumishi 2014 inaonyesha baraka za Yehova na bidii nyingi iliyoonyeshwa katika huduma. Kilele kipya cha wahubiri 6,737 kiliripotiwa katika mwezi wa Agosti. Pia kulikuwa na vilele vipya katika idadi ya magazeti na mafunzo ya Biblia. Kwa ujumla, katika mwaka wa utumishi wa 2014 kumekuwa na ongezeko la asilimia 6 katika idadi ya wahubiri, asilimia 12 ya mafunzo ya Biblia, na inatia moyo sana kuona ongezeko la asilimia 35 ya mapainia wasaidizi, na watu 566 walibatizwa.