Ratiba ya Juma Linaloanza Aprili 20
JUMA LINALOANZA APRILI 20
Wimbo 3 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 23 ¶10-18 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 23-25 (Dak. 8)
Na. 1: 1 Samweli 23:13-23 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Biblia Inaahidi Nini Kuhusu Wakati Ujao?—igw uku. 16 ¶1-3 (Dak. 5)
Na. 3: Binadamu Hakuandikiwa Kimbele Yatakayompata—td 14A (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: Tembeeni kama watu wenye hekima kwa ‘kujinunulia wakati unaofaa.’—Efe. 5:15, 16.
Dak. 15: “Jinsi ya Kutoa Ushahidi kwa Kutumia Meza na Vigari Vyenye Machapisho.” Mazungumzo. Panga kuwe na onyesho. Wahubiri wawili wanasimama kando ya meza au kigari chenye machapisho. Mhubiri mmoja anatabasamu anapomwona mpita-njia. Mhubiri yule mwingine pia anatabasamu anapomwona mpita-njia anayefuata, na mtu huyo anapokaribia anamuuliza swali, na kuanzisha mazungumzo kwa uchangamfu. Tunawezaje kutumia mfikio huu hata ikiwa hatutumii meza au vigari vyenye machapisho?
Dak. 15: Jambo Linalodumu la Ibada Yetu. Mazungumzo yanayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi Novemba 1, 2006, ukurasa wa 30-31, fungu la 14-17. Watie moyo wote waendelee kuhudhuria mikutano kwa ukawaida bila kuacha. Soma Waebrania 10:24, 25 na uonyeshe faida za kufanya hivyo.
Wimbo 75 na Sala