Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Tunatiwa moyo kuona kwamba kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia inaendelea vizuri huku wahubiri wakiongoza wastani wa mafunzo ya Biblia 1.1 katika mwezi wa Novemba.
Sudan: Katika mwezi wa Novemba, wahubiri wanne walibatizwa na mafunzo ya Biblia 1,498 yaliongozwa. Hiyo ni ishara nzuri ya kwamba kutakuwa na ongezeko zaidi.
Sudan Kusini: Wahubiri wanafanya kazi kwa bidii licha ya hali ngumu katika nchi hiyo. Tunashangalia pamoja na wale 25 waliobatizwa mwezi wa Novemba.
Tanzania: Inatia moyo kuona kwamba asilimia 15 ya wahubiri wote walishiriki katika aina moja au nyingine ya utumishi wa painia mwezi wa Novemba. Wahubiri waliongoza mafunzo 3,437 zaidi ikilinganishwa na mwezi huo mwaka wa 2013. Wastani wa mafunzo ya Biblia 1.3 yaliongozwa.