Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 8
JUMA LINALOANZA JUNI 8
Wimbo 6 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 25 ¶17-21, sanduku kwenye uku. 259 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 19-21 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Samweli 19:24-37 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Unawezaje Kuwa na Furaha?—igw uku. 22 ¶1-3 (Dak. 5)
Na. 3: Je, Mungu Anaona Kuna “Wema Katika Dini Zote”?—td 4D (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: “Kumbuka siku za kale.”—Kum. 32:7.
Dak. 10: “Kumbuka Siku za Kale.” Hotuba inayotegemea kichwa cha mwezi wa Juni. Soma na uzungumzie Kumbukumbu la Torati 4:9 na 32:7 na vilevile Zaburi 71:15-18. Eleza jinsi waeneza-injili wa siku hizi wanavyoweza kunufaika kwa kuwakumbuka watu na matukio yaliyopita ya kitheokrasi. Watie moyo wote kwamba mara kwa mara wanaweza kuzungumzia mfululizo wa makala katika Mnara wa Mlinzi zenye kichwa “Kutoka Katika Hifadhi ya Vitu Vyetu vya Kale” wakati wa Ibada ya Familia. Pitia baadhi ya sehemu za Mkutano wa Utumishi za mwezi huu, na uzungumzie jinsi zinavyohusiana na kichwa hicho.
Dak. 20: “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuanzisha Funzo la Biblia Mlangoni kwa Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!” Mazungumzo. Sehemu hii ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Pitia sehemu za ripoti ya utumishi wa shambani ya kutaniko zinazoonyesha kwamba kuna uwezekano wa kuwa na mafunzo zaidi ya Biblia. Panga kuwe na onyesho la mhubiri mwenye uzoefu akitumia pendekezo lililo kwenye sanduku kuanzisha funzo la Biblia mlangoni. Watie moyo wote waanzishe funzo la Biblia mlangoni.
Wimbo 29 na Sala