Ratiba ya Juma Linaloanza Juni 15
JUMA LINALOANZA JUNI 15
Wimbo 77 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 26 ¶1-9 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 22-24 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Samweli 22:21-32 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Ni Nani Watakaofufuliwa?—td 35A (Dak. 5)
Na. 3: Upendo na Utii Huleta Furaha—igw uku. 22 ¶4-6 (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: “Kumbuka siku za kale.”—Kum. 32:7.
Dak. 12: Ni Mtu Gani Anayetajwa Katika Biblia Unayempenda Zaidi? Mahojiano na hotuba. Anza kwa kuwahoji watoto wawili au watatu. Ni mtu gani anayetajwa katika Biblia wanayempenda zaidi? Biblia inasema alifanya nini? Wangependa kumwiga mtu huyo jinsi gani? Halafu, endelea na hotuba kuhusu jinsi watoto wanavyoweza kufaidika kutokana na kadi za wahusika katika Biblia zilizo kwenye jw.org/sw. (Angalia chini ya MAFUNDISHO YA BIBLIA > WATOTO.) Kila kadi ya mhusika katika Biblia inatia ndani picha na mambo machache kumhusu, ramani ya mahali alipoishi, mfuatano wa matukio unaoonyesha wakati alioishi, na maswali matatu kuhusu mtu huyo, na majibu ya maswali hayo. Kila kadi imetengenezwa kwa njia ambayo inaweza kuchapishwa na kuhifadhiwa. Watie moyo wazazi watumie sehemu hiyo kuwafundisha watoto wao kuhusu “siku za kale.”—Kum. 32:7.
Dak. 18: “Kujifunza Kutoka kwa Wahubiri Wenye Uzoefu Zaidi.” Mazungumzo. Mnapozungumzia fungu la pili, waombe wasikilizaji waeleze jinsi walivyofaidika walipokuwa wakihubiri pamoja na mhubiri mwenye uzoefu.
Wimbo 4 na Sala