Ratiba ya Juma Linaloanza Julai 27
JUMA LINALOANZA JULAI 27
Wimbo 18 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 28 ¶1-9 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Wafalme 15-17 (Dak. 8)
Na. 1: 1 Wafalme 15:16-24 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Biblia Inaweza Kuwasaidiaje Wake?—igw uku. 26 ¶3-4 (Dak. 5)
Na. 3: Wakristo Hawakupewa Sheria ya Sabato—td 28B (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: “Nendeni mkafanye wanafunzi.”—Mt. 28:19, 20.
Dak. 10: Je, Unaboresha Ustadi Wako Katika Huduma? Mazungumzo. Zungumzia fungu la kwanza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2014, ambalo linaonyesha kusudi la mfululizo, “Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma.” Zungumzia kwa ufupi makala za awali. Waombe wasikilizaji waeleze faida hususa ambazo wamepata kupitia mfululizo huo. Watie moyo wasikilizaji wazingatie jambo linalokaziwa kila mwezi kwa kutumia mapendekezo yaliyo chini ya kichwa, “Jaribu Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima.”
Dak. 10: Tumia Kijitabu Utangulizi wa Neno la Mungu—Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia. Mazungumzo. Zungumzia jinsi tunavyoweza kutumia mambo yafuatayo kumsaidia mwanafunzi wa Biblia aitumie Biblia kwa njia nzuri: (1) “Jinsi ya Kupata Mistari ya Biblia.” (2) Swali la 19: “Vitabu vya Biblia vina ujumbe gani?” (3) Swali la 20: “Unawezaje kunufaika zaidi unaposoma Biblia?” Panga kuwe na onyesho fupi la mhubiri akizungumzia pamoja na mwanafunzi wake mojawapo ya mambo hayo baada ya kumaliza funzo.
Dak. 10: “Vifaa Vyetu vya Kufundishia.” Maswali na majibu.
Wimbo 125 na Sala