Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/15 uku. 3
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 12/15 uku. 3

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 28, 2015. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.

  1. Je, Daudi aliwatendea kikatili mateka wake kama wengine wanavyokata kauli kutokana na 1 Mambo ya Nyakati 20:3? [Nov. 2, w05 2/15 uku. 27]

  2. Ni nini kilimchochea Daudi kuonyesha ukarimu, na ni nini kitatusaidia kumwiga? (1 Nya. 22:5) [Nov. 9, w05 10/1 uku. 11 fu. 7]

  3. Daudi alimaanisha nini alipomwambia Sulemani: “Mjue Mungu wa baba yako”? (1 Nya. 28:9) [Nov. 16, w10 11/1 uku. 30 fu. 3, 7]

  4. Ombi la Sulemani katika andiko la 2 Mambo ya Nyakati 1:10 linaonyesha nini kumhusu, na tunaweza kujifunza nini kwa kuchunguza sala zetu za kibinafsi kwa Yehova? (2 Nya. 1:11, 12) [Nov. 23, w05 12/1 uku. 19 fu. 6]

  5. Kulingana na andiko la 2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30, Yehova ana uwezo gani wa pekee, na kwa nini tummiminie moyo wetu katika sala? (Zab. 55:22) [Nov. 30, w10 12/1 uku. 11 fu. 7]

  6. Asa aliomba ushindi juu ya jeshi lenye watu wengi kwa msingi gani, na tunaweza kuwa na uhakika gani kuhusiana na vita vyetu vya kiroho? (2 Nya. 14:11) [Des. 7, w12 8/15 uku. 8 fu. 6–uku. 9 fu. 1]

  7. Jinsi ambavyo Yehova alishughulika na udhaifu wa Mfalme Yehoshafati kunatuhakikishiaje upendo wa Mungu, na hilo linapaswa kuathirije maoni yetu kuelekea wengine? (2 Nya. 19:3) [Des. 14, w03 7/1 uku. 17 fu. 13; cl uku. 245 fu. 12]

  8. Ni kwa nini tunapaswa ‘kusimama mahali petu’ na ‘kusimama tuli’ katika siku zetu, na tunawezaje kufanya hivyo? (2 Nya. 20:17) [Des. 21, w05 12/1 uku. 21 fu. 3; w03 6/1 uku. 21 fu. 15-16]

  9. Tunaposoma andiko la 2 Mambo ya Nyakati 21:20, tunapata somo gani la kusikitisha kuhusiana na kifo cha Yehoramu? [Des. 21, w98 11/15 uku. 32 fu. 4]

  10. Kulingana na 2 Mambo ya Nyakati 26:5, ni nani aliyekuwa kielelezo kizuri kwa Uzia, na vijana leo wanaweza kupata manufaa gani kutoka kwa Wakristo wakomavu kutanikoni? [Des. 28, w07 12/15 uku. 10 fu. 2, 4]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki