Sanduku La Swali
◼ Ni nini kinachoweza kumfanya mhubiri asitishe funzo la Biblia?
Mwanafunzi akiacha kufanya maendeleo ya kiroho, huenda ukalazimika kuacha kujifunza naye Biblia kwa busara. (Mt. 10:11) Jiulize: Je, anapatikana wakati mliokubaliana kujifunza? Je, anatayarisha mapema kwa ajili ya funzo lake? Je, amehudhuria mikutano yoyote ya kutaniko? Je, anawaeleza wengine mambo anayojifunza? Anafanya mabadiliko kupatana na kanuni za Biblia? Bila shaka, tunapaswa kuzingatia umri na uwezo wake, na kukumbuka kwamba baadhi ya wanafunzi wanaweza kufanya maendeleo haraka na wengine wanaweza kuchukua muda mrefu. Pia, unapoamua kusitisha funzo hakikisha kwamba mwanafunzi anatambua kuwa uko tayari kujifunza naye ikiwa atataka kuendeleza funzo lake wakati ujao.—1 Tim. 2:4.