Januari 4-10
2 MAMBO YA NYAKATI 29-32
Wimbo 114 na Sala
Utangulizi (Isizidi dak. 3)
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
“Jitihada Nyingi Zinahitajiwa Ili Kuendeleza Ibada ya Kweli”: (Dak. 10)
2Nya 29:10-17—Hezekia alikuwa mwenye bidii katika kurudisha ibada ya kweli
2Nya 30:5, 6, 10-12—Hezekia anawakaribisha watu wote wenye mioyo minyoofu wakusanyike kwa ajili ya ibada
2Nya 32:25, 26—Hezekia anaacha majivuno na kuwa mnyenyekevu (w05 10/15 25 ¶20)
Kutafuta Hazina za Kiroho: (Dak. 8)
2Nya 29:11—Hezekia aliwekaje mfano mzuri kuhusiana na mambo aliyotanguliza? (w13 11/15 17 ¶6-7)
2Nya 32:7, 8—Ni hatua gani inayofaa zaidi tunayoweza kuchukua ili kujitayarisha kwa ajili ya hali ngumu za wakati ujao? (w13 11/15 20 ¶17)
Usomaji wa Biblia wa juma hili unanifundisha nini kumhusu Yehova?
Ni mambo gani katika usomaji wa Biblia wa juma hili ninayoweza kutumia katika huduma ya shambani?
Usomaji wa Biblia: 2Nya 31:1-10 (Isizidi dak. 4)
BORESHA HUDUMA YAKO
Uwe Tayari Kutoa Machapisho Mwezi Huu: (Dak. 15) Mazungumzo. Onyesha sehemu ya kwanza ya video ya Mapendekezo ya Kutoa Mnara wa Mlinzi, halafu uzungumzie mambo makuu. Kazia jinsi mhubiri alivyoweka msingi wa ziara ya kurudia. Fanya vivyo hivyo pia ukitumia sehemu ya pili ya video ya Mapendekezo ya Kutoa Mnara wa Mlinzi na broshua Habari Njema. Rejelea makala yenye kichwa “Jinsi ya Kuongoza Funzo kwa Kutumia Broshua Habari Njema.” Watie moyo wahubiri waandike utangulizi wao wenyewe. Ikiwa video hiyo haipatikani, panga kuwe na onyesho.
MAISHA YA MKRISTO
“Pendeleo Letu la Kujenga na Kudumisha Majumba ya Ibada ya Kweli”: (Dak. 15) Mazungumzo. Waombe wale ambao wamewahi kushiriki katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme wasimulie jinsi walivyopata shangwe. Mhoji kwa ufupi ndugu ambaye husimamia usafi na udumishaji wa Jumba la Ufalme kuhusu mipango ya kutaniko.
Funzo la Biblia la Kutaniko: ia sura ya 6 ¶1-14 (Dak. 30)
Pitia Mambo Makuu Ambayo Mmejifunza, na Mtakayojifunza Juma Linalofuata (Dak. 3)
142 na Sala
Kikumbusho: Tafadhali sikilizeni kwanza muziki, kisha mwimbe wimbo huo mpya.