Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Oktoba uku. 3
  • Jinsi ya Kuwa Mwanafunzi Mwenye Bidii wa Maandiko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwa Mwanafunzi Mwenye Bidii wa Maandiko
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Je, Kweli Mungu Anakujali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Jinsi Kitabu Cha Danieli Kinavyokuhusu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Kuwatambua Waabudu wa Kweli Katika Wakati wa Mwisho
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Oktoba uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kuwa Mwanafunzi Mwenye Bidii wa Maandiko

Je, ungependa kuwa mwaminifu unapokabili majaribu kama Danieli alivyokuwa? Danieli alijifunza kwa bidii Neno la Mungu, kutia ndani unabii wenye kina. (Da 9:2) Kujifunza Biblia kwa bidii kunaweza kukusaidia kudumisha uaminifu. Jinsi gani? Kunaweza kuongeza imani yako kwamba ahadi za Yehova zitatimia. (Yos 23:14) Pia kunaweza kukusaidia kuongeza upendo wako kwa Mungu, ambao utakuchochea kufanya yaliyo sawa. (Zb 97:10) Lakini unapaswa kuanzia wapi? Fikiria mapendekezo yafuatayo.

Danieli akijifunza Neno la Mungu
  • Ninapaswa kujifunza nini? Ratiba nzuri ya kujifunza inatia ndani kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. Usomaji wa Biblia wa kila juma utakuwa na faida zaidi kwako ikiwa utatenga wakati wa kufanya utafiti kuhusu mambo ambayo hujaelewa. Isitoshe, wengine wamechagua kujifunza mambo mengi zaidi kuhusu unabii wa Biblia, sifa za tunda la roho ya Mungu, safari za umishonari za mtume Paulo, au hata uumbaji wa Yehova. Ukifikiria swali fulani la Biblia unapoendelea na shughuli za kila siku, liandike na ulifanye liwe mradi unaofuata wa funzo lako la kibinafsi.

  • Ninaweza kupata wapi habari? Ili upate mapendekezo kadhaa, tazama video Vifaa vya Utafiti Vinavyotusaidia Kupata Hazina za Kiroho. Ili kupima uwezo wako wa kufanya utafiti, chunguza kuhusu serikali kuu za ulimwengu zinazofananishwa na wanyama kwenye Danieli sura ya 7.

  • Ninapaswa kutumia muda gani kujifunza? Ili kuwa na afya kiroho ni muhimu sana kuwa na funzo la kawaida. Unaweza kuanza na vipindi vifupi vya kujifunza, kisha uongeze muda huo hatua kwa hatua. Kujifunza Neno la Mungu ni kama kuchimba hazina zilizofichika; kadiri unavyopata hazina nyingi, ndivyo utakavyokuwa na hamu ya kuchimba zaidi! (Met 2:3-6) Hamu yako ya kujifunza Neno la Mungu itaongezeka, na funzo la Biblia la ukawaida litaendelea kuwa sehemu ya ratiba yako.​—1Pe 2:2.

    Kwa mapendekezo zaidi ya jinsi ya kufanya funzo liwe lenye kufurahisha, ona gazeti la Amkeni! la Februari 2012, uku. 18-​20.

WANYAMA WANAOTAJWA KWENYE DANIELI SURA YA 7 WANAWAKILISHA NINI?

  • Mnyama aliye kama simba mwenye mabawa ya tai

    Da 7:4

  • Mnyama aliye kama dubu mwenye mifupa mitatu ya mbavu kinywani

    Da 7:5

  • Mnyama aliye kama chui mwenye vichwa vinne na mabawa manne

    Da 7:6

  • Mnyama mwenye kutisha aliye na meno ya chuma na pembe kumi

    Da 7:7

SWALI LA ZIADA:

Unabii wa Danieli 7:​8, 24 ulitimizwaje?

Pembe ndogo iliyo na macho na kinywa ikitokea kati ya zile pembe kumi na kung’oa pembe tatu

MRADI UNAOFUATA:

Wanyama wanaotajwa kwenye Ufunuo sura ya 13 wanawakilisha nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki