Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
OKTOBA 2-8
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | DANIELI 7-9
it-2 902 ¶2
Majuma Sabini
Kukomesha makosa na dhambi. Kuuawa kwa Yesu, kufufuliwa kwake, na kwenda kuonekana mbinguni ‘kulikomesha makosa, kukamaliza kabisa dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya kosa.’ (Da 9:24) Agano la Sheria lilikuwa limefunua kwamba Wayahudi ni watenda-dhambi, likawahukumu, na kuwalaani kwa kuvunja agano. Lakini mahali ambapo dhambi “ilizidi” kama ilivyofunuliwa au kuthibitishwa na Sheria ya Musa, rehema za Mungu na kibali chake kilizidi kupitia Masihi wake. (Ro 5:20) Kupitia dhabihu ya Masihi, makosa na dhambi za watenda-dhambi waliotubu zinaweza kufutwa na adhabu ya dhambi hizo kuondolewa.
it-2 900 ¶7
Majuma Sabini
Kutokea kwa Masihi Baada ya Majuma ‘Sitini na Tisa.’ Yale “majuma sitini na mbili” yaliyofuata (Da 9:25), yangeanza baada ya kukamilika kwa yale “majuma saba” kwa kuwa yalikuwa sehemu ya yale majuma 70 lakini yalikuwa ya pili kutajwa. Kwa hiyo, tangu “kutolewa kwa lile neno” la kujenga upya Yerusalemu mpaka “Masihi aliye Kiongozi” kungekuwa na “majuma” 7 kuongeza 62, au “majuma” 69, yaani, miaka 483, kuanzia mwaka wa 455 K.W.K. hadi 29 W.K. Kama ilivyotajwa tayari, katika majira ya vuli ya mwaka wa 29 W.K., Yesu alibatizwa katika maji, akatiwa mafuta kwa roho takatifu, na kuanza huduma yake akiwa “Masihi aliye Kiongozi.”—Lu 3:1, 2, 21, 22.
it-2 901 ¶2
Majuma Sabini
‘Akatiliwa mbali’ katikati ya juma. Gabrieli aliendelea kumwambia Danieli hivi: “Baada ya yale majuma 62 Masihi atakatiliwa mbali, bila kuwa na chochote kwa ajili yake.” (Da 9:26) Muda fulani baada ya kukamilika kwa yale ‘majuma saba kuongeza sitini na mbili,’ yaani baada ya miaka mitatu na nusu, Kristo aliuawa kwenye mti wa mateso, akitoa kila kitu alichokuwa nacho kiwe dhabihu kwa ajili ya wanadamu. (Isa 53:8) Uthibitisho unaonyesha kwamba Yesu alitumia nusu ya kwanza ya “juma” hilo katika huduma. Pindi moja, huenda wakati wa masika ya mwaka wa 32 W.K., alitoa mfano, na inaonekana alikuwa akilinganisha taifa la Kiyahudi na mtini (Linganisha na Mt 17:15-20; 21:18, 19, 43) ambao haukuzaa matunda yoyote kwa “miaka mitatu.” Mtunza-mizabibu alimwambia hivi mmiliki wa shamba la mizabibu: “Bwana, uache mwaka huu pia, mpaka niupalilie na kuweka mbolea; na ndipo ukizaa matunda wakati ujao, basi ni vema; lakini ikiwa sivyo, utaukata.” (Lu 13:6-9) Inawezekana kwamba hapa alikuwa akirejelea kipindi cha huduma yake katika taifa hilo lisilowajibika, huduma ambayo kufikia wakati huo alikuwa ameifanya kwa miaka mitatu na ambayo ingeendelea katika mwaka wa nne.
it-2 901 ¶5
Majuma Sabini
“Nusu ya juma” ingekuwa katikati ya miaka saba, au baada ya miaka mitatu na nusu ndani ya “juma” hilo la miaka. Kwa kuwa “juma” la 70 lilianza wa masika ya mwaka wa 29 W.K. wakati ambapo Yesu alibatizwa na kutiwa mafuta kuwa Kristo, hivyo, nusu ya juma hilo (miaka mitatu na nusu) ingeendelea hadi wakati wa majira ya kuchipua ya mwaka wa 33 W.K., au wakati wa Pasaka (Nisani 14) ya mwaka huo. Kulingana na kalenda ya Gregory siku hiyo ilikuwa Aprili 1, 33 W.K. (Ona LORD’S EVENING MEAL [Time of Its Institution].) Mtume Paulo alisema kwamba Yesu ‘alikuja ili kufanya mapenzi ya Mungu,’ ambayo yalikuwa ‘kuondolea mbali lile la kwanza [yaani, dhabihu na matoleo yaliyoonyeshwa katika Sheria] ili asimamishe lile la pili.’ Alifanya hivyo kwa kutoa mwili wake mwenyewe kuwa dhabihu.—Ebr 10:1-10.