Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Juni uku. 8
  • Wazazi, Wazoezeni Watoto Wenu Vizuri Ili Wafanikiwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazazi, Wazoezeni Watoto Wenu Vizuri Ili Wafanikiwe
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Juni uku. 8
Yosefu na Maria wakitumia wakati wa mlo kumfundisha Yesu na watoto wao wengine

MAISHA YA MKRISTO

Wazazi, Wazoezeni Watoto Wenu Vizuri Ili Wafanikiwe

Wazazi wanaomwogopa Mungu wana hamu ya kuwaona watoto wao wakiwa watumishi waaminifu wa Yehova. Wazazi wanaweza kuwasaidia kwa kukazia mafundisho ya Biblia mioyoni mwao tangu wanapokuwa watoto wachanga. (Kum 6:7; Met 22:6) Je, wazazi wanahitaji kujidhabihu ili wafanye hivyo? Bila shaka! Lakini jitihada zao zitathawabishwa sana.—3Yo 4.

Wazazi wanaweza kujifunza mambo mengi kutoka kwa Yosefu na Maria. “Walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya sherehe ya Pasaka,” hata ingawa kufanya hivyo kulihitaji jitihada na gharama. (Lu 2:41) Jambo muhimu zaidi maishani mwao lilikuwa hali ya kiroho ya familia yao. Vivyo hivyo, wazazi leo wanaweza kuwasaidia watoto wao kuchukua hatua zinazofaa kwa kutumia kila fursa kuwafundisha kwa maneno na kwa mfano wao.—Zb 127:3-5.

JE, WAJUA?

Ingawa ndugu nusu wa Yesu walilelewa katika familia ya kiroho, hawakumwamini hadi baada ya kifo chake. (Yoh 7:5; Mdo 1:14) Baadaye, wawili kati yao, Yakobo na Yuda, waliandika vitabu vya Biblia.

TAZAMENI VIDEO WALITUMIA KILA FURSA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Jon na Sharon Schiller walitangulizaje mambo ya Ufalme walipokuwa wakiwalea watoto wao?

  • Kwa nini wazazi wanapaswa kumpa kila mtoto nidhamu kulingana na uhitaji wake?

  • Wazazi wanaweza kuwatayarishaje watoto wao kukabiliana na majaribu ya imani?

  • Umetumia vifaa gani vinavyoandaliwa na tengenezo la Yehova ili kuwasaidia watoto wako kukua kiroho?

Familia ya Schiller

Hakikisha kwamba familia yako inatanguliza mambo ya kiroho

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki