Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Agosti uku. 7
  • Yesu Alikufa kwa Ajili ya Ndugu Yako Pia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Alikufa kwa Ajili ya Ndugu Yako Pia
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Endelea Kuwa na Mtazamo wa Akili wa Kristo Ndani Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Msiwakwaze “Hawa Wadogo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Samehe Kutoka Katika Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
mwb18 Agosti uku. 7
Yesu akizungumza na wafuasi wake

MAISHA YA MKRISTO

Yesu Alikufa kwa Ajili ya Ndugu Yako Pia

Yesu alidhabihu uhai wake kwa ajili ya watu wasio wakamilifu. (Ro 5:8) Bila shaka, sisi binafsi tunathamini kwamba Yesu alituonyesha upendo kwa kutoa uhai wake kwa ajili yetu. Hata hivyo, nyakati nyingine huenda tukahitaji kujikumbusha kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya ndugu yetu pia. Tunaweza kuwaonyeshaje ndugu na dada zetu upendo kama wa Kristo, kwa kuwa kama sisi wao pia si wakamilifu? Fikiria njia tatu. Kwanza, tunaweza kuongeza marafiki kutia ndani wale ambao wana malezi tofauti na yetu. (Ro 15:7; 2Ko 6:12, 13) Pili, tunaweza kuwa waangalifu tusiseme au kufanya mambo yanayoweza kuwaudhi wengine. (Ro 14:13-15) Mwishowe, mtu akitutendea dhambi, tunaweza kumsamehe haraka. (Lu 17:3, 4; 23:34) Tukijitahidi sana kumwiga Yesu katika njia hizo, Yehova ataendelea kubariki kutaniko kwa amani na umoja.

TAZAMENI VIDEO BORESHA UTU WAKO WA KIKRISTO!, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Miki akikaribishwa katika kutaniko lake jipya

    Mwanzoni Miki alihisije kuhusu kutaniko lake?

  • Miki akikasirishwa na wengine kutanikoni

    Ni nini kilichofanya hisia zake zibadilike?

  • Yesu anawatendea kwa fadhili mitume wake hata ingawa walilala

    Mfano wa Yesu ulimsaidiaje Miki kubadili mtazamo wake? (Mk 14:38)

  • Miki akicheka baada ya mvulana mdogo kumgonga na kumfanya ajimwagie kinywaji chake nguoni

    Methali 19:11 inaweza kutusaidiaje kuwa na maoni yanayofaa kuwahusu Wakristo wenzetu?

MAMBO YA KUTAFAKARI:

Je, ninashikilia makosa fulani hususa niliyotendewa na Mkristo mwenzangu ambayo ninapaswa kuachilia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki